Thursday, December 28, 2017

FAHAMU KUHUSIANA NA CHANGO LA UZAZI.

Tunapozungumzia mgonjwa wa chango tuna maana kuwa ni matatizo yaliyopo katika viungo vya uzazi kwa mke au mume. Huu ni ugonjwa ambao humpata mtu katika umri mdogo utotoni. Kwa mfano :- mume, hupata maumivu ya tumbo mara kueneza anapokuwa mdogo. Kwa upande wa mwanamke hupata maumivu ya tumbo anapoanza kuvunja ungo. Maumivu hayo hupelekea mtu (mume/mwanamke) kupata madhara katika viungo vyake vya uzazi.

DALILI ZAKE

Kwa mwanaume atakuwa akishiriki tendo la ndoa, anawahi sana kufika kileleni na kurudia mara nyingine ni vigumu sana.Pia mwanaume hatakuwa na uwezo wa kusimamisha.Ni vigumu kumpa mimba mwanamke.
Mwanamke mwenye chango la uzazi ana dalili zifuatazo:-

Kupata maumivu makali wakati anapokaribia kuingia katika siku zake za hedhiKuhisi maumivu makali wakati wa kushiriki tendo la ndoaSiku zake za hedhi hazitakuwa na ratiba, zitakuwa zinabadilika badilikaHujisikia homa kali anapokaribia siku zake za dhedhiKupatwa hasirakali/ jazba anapokaribia kuingia katika siku zake za hedhi.Kujisikia uchovu mkubwa anapokaribia siku zake za hedhi.Kupata mchubuko kwenye mapaja na sehemu za uke.Kuchukia kushiriki tendo la ndoaKupata uvimbe kwenye kizaziMimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi
Madhara yake kwa mwanamke

Kwa mwanamke ni vigumu kupata mimbaMwanaamke anaweza kuwa tasa kabisaKuingia na kutoka kwa mimbaKuwa na hamu ya tendo la ndoa lakini hafikii kileleniKuwa na uke mdogo sana

Madhara kwa Mwanaume

Kuwa na mbegu ambazo haziwezi kutunga mimbaKiwango kinachozalishw cha megu ni kidogo mnoKuwa na kiwewe cha kushiriki tendo la ndoaKusimama na kusinyaa kwa uume

Tiba ya Chango la Uzazi 

Ni vizuri sana kumweleza Dr. Dalili zote mtu anapojisikia.
Mara nyingi ugonjwa huu hautibiwi kwa dawa za hospitalini, bali ugonjwa wa chango la uzazi hutibiwa na miti shamba.
Dawa inayotibu ugonjwa huu ni dawa inayotibu kizazi.Matumizi yake kawaida mtu ataitumia kulingana na ukubwa wa tatizo lake.
Huchanganywa na viungo vya uzazi vya wanyama, ambavyo kazi yake ni kuondoa matatizo yaliyopo, kwenye kizazi cha manamke/mwanaume.
Wengi wana amini kuwa dawa za miti shamba hazina uwezo wa kutibu haya ni mawazo potofu, miti shamba ndiyo suluhisho la kila tatizo katika afya zetu.
Mimi mwenyewe ni shuhuda nimelelewa katika miti shamba, ukipewa dawa ya mitishamba haijakusaidia ufahamu kuwa kiwango cha Dr/Mganga huyo hakijakomaa

Saturday, December 23, 2017

Homoni zina mchango mkubwa katika afya kwa ujumla katika mwili wa mwanamke hasa linapokuja suala la uzazi. Mara nyingi usawa usio sawa wa homoni husababishwa na mabadiliko katika homoni ya ‘estrogen’.

Mabadiliko haya mara nyingi hutokea wakati wa kuvunja ungo, wakati wa hedhi, wakati wa ujauzito na wakati wa ukomo wa hedhi (menopause).

Vitu vingine vinavyopelekea mabadiliko ya homoni ni pamoja na kuongezeka umri, lishe duni, kutokujishughulisha na mazoezi, kupungua kwa ogani ya adreno, mfadhaiko au stress, kukosa usingizi, dawa za uzazi wa mpango, sumu na kemikali mbalimbali nk.
Wanawake wengi hukata tamaa ya kupata mtoto kwa kudhani Ni wagumba kumbe wakati mwingine  huwa Ni tatizo LA homoni imbalance .
sasa utajuaje unahomoni imbalance!? Na je, ufanyeje!?

Dalili zitakazokuonyesha homoni zako hazipo sawa ni pamoja na:

1. Kuwa na tabia ya hamaki (kukosa utulivu)
2. Uchovu sugu
3. Kuongezeka uzito
4. Kupungua kwa nywele
5. Maumivu ya kichwa ya mara kwa mara
6. Kukosa hamu ya tendo la ndoa
7. Chunusi
8. Kuwa na hamu na vyakula au vinywaji vya viwandani kila mara
9. Kushindwa kushika ujauzito
10. Kutokujisikia vizuri kila mara bila sababu maalumu
11. Kukosa usingizi
12. Hasira zisizo na sababu maalumu nk

Zipo dawa za asili zinazoweza kukusaidia kurekebisha na hatimaye kuweka sawa usawa wa homoni mwilini mwako.

Ni mhimu uonane na daktari kabla kwa uchunguzi, vipimo na ushauri zaidi kabla ya kuamua kutumia hivi vinavyopendekezwa kwenye makala hii hasa kama una matatizo kama ya uvimbe katika kizazi, saratani ya matiti, saratani ya kizazi au una saratani katika mirija ya uzazi.

Njia mbadala 6 za kurekebisha homoni zako na hatimaye upate ujauzito:

1. TUMIA OMEGA 3 KILA SIKU

Asidi mafuta yenye Omega-3 yana umhimu mkubwa katika kuweka sawa homoni zako.

Kwa wanawake yana umhimu mkubwa kwani husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi usiosawa na kupunguza dalili za kukoma kwa hedhi (menopausal symptoms). Omega-3 husaidia kuondoa sumu mwilini na vivimbe sehemu mbalimbali za mwili.

• Vitu vyenye omega 3 kwa wingi ni pamoja na mafuta ya samaki (yasiyo na mercury), walnuts, maharage ya soya, mafuta ya nazi, mafuta ya zeituni, mafuta ya mawese na mbegu za maboga. Tumia hivi vitu kila siku katika kuishi kwako ili kuweka sawa homoni zako.

2. VITAMINI D

Vitamini D ni mhimu kwa ajili ya tezi ya pituitari (pituitary gland) iweze kufanya kazi zake vizuri na ni tezi inayotengeneza homoni zingine nyingi mhimu.

Vitamini D pia husaidia kuondoa dalili zinazohusiana na usawa mdogo wa homoni ya ‘estrogen’. Vitamini D pia ina uhusiano na kiwango cha njaa ulichonacho na uzito pia.

Upungufu wa vitamini D unaweza pia kupelekea utolewaji usiosawa wa homoni nyingine ijulikanayo kama ‘parathyroid’.

• Tembea juani wakati wa jua kali dakika 20 hadi 30 kila siku huku ukiwa wazi sehemu kubwa ya mwili wako.

• Kula vyakula kama mafuta ya samaki, maziwa na mayai ya kuku wa kienyeji kila siku.

3. JISHUGHULISHE NA MAZOEZI YA VIUNGO

Kujishughulisha na mazoezi ya viungo ndiyo njia rahisi ya kurekebisha homoni zako kwani mazoezi yanahusika katika uzalishaji wa hizo homoni. Mazoezi huipunguza nguvu homoni inayohusika na mfadhaiko (stresss) ijulikanayo kwa kitaalamu kama ‘cortisol’.

Hii homoni ya Cortisol huidhibiti homoni nyingine mhimu ijulikanayo kama ‘estrogen’ ambayo kama itazidi basi inaweza kuleta madhara kwa afya yako yote kwa ujumla.

Mazoezi ya mara kwa mara huusaidia ubongo kutoa kemikali ambazo huongeza hali ya kujisikia vizuri (improves your mood). Jambo hili la kupelekea ujisikie vizuri husaidia kuweka sawa homoni zako.

Siyo hilo tu mazoezi yatakusaidia pia kuwa na uzito sahihi kwani uzito uliozidi ni sababu mojawapo inayopelekea homoni zako kutokuwa sawa.

Nusu saa ya mazoezi kwa siku inatosha. Tatizo wanawake wengi hawana habari na kitu kinaitwa mazoezi!

• Nenda kaogelee, katembee kwa miguu lisaa limoja, au kimbia taratibu (jogging) mara 3 mpaka 4 kwa wiki.

4. TUMIA MAFUTA YA NAZI

Mafuta ya nazi yale ya asili yaliyotengenezwa nyumbani bila kupita kiwandani ni dawa nyingine nzuri ya asili ya kurekebisha na kuweka sawa homoni zako. Mafuta haya huiwezesha tezi ya koromeo (thyroid) kufanya kazi zake vizuri.

Mafuta ya nazi pia husaidia kuweka sawa sukari katika damu, huongeza kinga ya mwili, huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kusaidia pia kupunguza uzito. Mafuta haya ni mazuri kwa afya ya moyo wako na hayana kolesto yoyote mbaya.

Kunywa vijiko vikubwa viwili kila siku kwa mwezi mmoja hata miwili au hata mitatu kwa uhakika wa matokeo mazuri zaidi. Unaweza pia kuyaweka kwenye kachumbali. Pia nakushauri kila upikapo wali tumia tui zito la nazi na siyo wali tu hata katika mapishi mengine unaweza kutumia tui la nazi, kazi ni kwako.

5. UWATU PIA HUREKEBISHA HOMONI

Madaktari wengi wa tiba asili duniani hushauri kutumia uwatu (kwa Kiingereza huitwa ‘fenugreeek’) kwa ajili ya kuongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha. Uwatu hutumika pia kama dawa ya asili ya kuongeza ukubwa wa matiti (natural breast enlargement).

Uwatu husaidia umeng’enywaji wa sukari mwilini na hivyo kuwa msaada mkubwa kwa watu wanaosumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na uzito kupita kiasi (obesity).

• Chukua kijiko kikubwa kimoja cha unga wa mbegu za uwatu na uweke ndani ya glasi moja ya maji ya uvuguvugu, koroga vizuri na unywe yote. Fanya hivi kutwa mara 2 kwa mwezi mmoja mpaka miwili.

Unaweza kuongeza asali kidogo kupata radha. Unaweza kutumia pia ndani ya maziwa ya moto hasa kama huna vidonda vya tumbo au kisukari.

6. TUMIA MREHANI (Basil)

Mrehani hutumika pia kama dawa ya asili ya kurekebisha homoni. Huiweka sawa homoni ya ‘cortisol’ ambayo kama itazidi kuwa nyingi inaweza kuleta shida kwenye homoni koromeo (thyroid gland), Mirija ya uzazi na Kongosho. Wakati huo huo mrehani husaidia kuweka sawa akili yako na hivyo huleta hali ya kujisikia vizuri (good mood).

Unaweza kupata Mrehani ukiwa Dar kwenye soko la kisutu au hata kariakoo pia Zanzibar. Ni kiungo mhimu katika mahoteli mengi ya kitalii.

• Tengeneza chai ukitumia majani fresh ya mmea huu na unywe kikombe kimoja kutwa mara 3 kwa miezi miwili hadi mitatu.

MAMBO YA MHIMU KUZINGATIA:

Pamoja na dawa, zingatia haya yafuatayo kwa matokeo mazuri zaidi:

• Kula parachichi 1 kila siku
• Tumia vyakula asili zaidi kuliko vya kwenye makopo na migahawani (fast foods)
• Tumia vyakula vyenye nyuzinyuzi (fiber) nyingi kwenye chakula chako
• Epuka kahawa, chai ya rangi, soda nyeusi na vinywaji vingine vyote vyenye kafeina ndani yake
• Achana na msongo wa mawazo (stress) na upate usingizi wa kutosha kila siku
• Usitumie dawa za uzazi wa mpango kama unahitaji kuweka sawa homoni zako
• Epuka vilevi vyote
• Kunywa maji mengi kila siku lita 2 hadi 3
• Usitumie vyakula vya moto kwenye vyombo vya plastiki

Monday, November 13, 2017

Ugonjwa wa mtoto kuzaliwa na nafasi kwenye uti wa mgongo unaitwa Spina Bifidaugonjwa huu hutokana na upungufu wa vitamin B9 (foliac acid).

mama mjamzito hutakiwa kutumia vitamin B9 wakati wa ujauzito au wakati anpopanga kuwa mjamzito. vit hivi huzsaidia kukuwa kwa neva na ubongo mwilini.Dalili ya kawaida ya upungufu wa Vit B9, Vitc ni pamoja na kuharisha, anemia na udhaifu au kupumua kwa taabu, uharibifu wa neva (mishipa ya fahamu)na mwili kuwa una kufa ganzi matatizo ya mimba, kuchanganyikiwa akili, usahaulifu au kumbukumbu kuwa ndogo, majonzi ya akili (depression), au vidonda katika ulimi, midomo , maumivu ya kichwa, mapigo ya moyo kwenda haraka , kuwashwa, na matatizo ya kitabia.

Kiwango cha chini cha Vit B9 na Vt C pia husababisha mkusanyiko homocysteine. DNA zisip okarabati huharibika na hii inaweza kusababisha maendeleo ya kansa.

Vyakula vyenye vitamini hii ni mboga za majani ya kijani, mbazi, choroko
Mama zingatia maelezo ya clinic ni muhimu. Kwa mengi zaidi tufuatilie kupitia www.afyanauzazi.blogspot com au tuffollow insta @afyanauzazi

Friday, October 20, 2017

 Image result for MADAWA HATARI KWA MJAMZITO
dawa ambazo jamii yetu huzitumia mara kwa mara kujitibu magonjwa mbalimbali na hupatikana kirahisi mtaani Lakini  bahati mbaya baadhi ya dawa hizo hazitakiwi kupewa kwa wajawazito kabisa kulingana na madhara makubwa yanayoambatana na dawa hizo kwa mtoto aliyepo tumboni.
Zifuatazo ni dawa hizo.

  • Albendazole; hii ni dawa ya minyoo ambayo hutumika mara kwa mara kujitibu lakini ni dawa mbaya sana kwa akina mama wajawazito kwani una uwezo wa kutoa mimba kabisa hivyo mebendazole hutumika kama mbadala.

  • Gentamycin: hii ni dawa ambayo iko kwenye mfumo wa sindano tu, mara nyingi hutumika kutibu magonjwa ya mfumo wa mkojo. Dawa hii huharibu kabisa mishipa ya fahamu kitaalamu kama auditory nerve ambayo hutufanya sisi kusikia. Hivyo matumizi ya dawa hii huweza kusababisha mototo kuzaliwa akiwa hasikii yaani kiziwi.

  • Ciproflaxin; hii ni dawa ambayo hupatikana kwenye mfumo wa vidonge na sindano, mara nyingi hutumika kutibu typhoid, UTI au magonjwa ya njia za mkojo na magonjwa baadhi ya zinaa. Dawa hii huharibu ukuuji wa mifupa ya mtoto na huweza kutoa mtoto asiyetembea mwishoni.

  • Doxycline: hii ni dawa ambayo hupatikana kwa mfumo wa dawa za kumeza kitaaalamu kama capsules, dawa hizi ni antibiyotiki yaani hutumika kuua bakteria wa aina tofauti. Bahati mbaya huweza kuingilia mfumo wa utengenezaji wa mtoto ikitumika miezi mitatu ya mwanzo na kusababisha kuzaliwa na motto mwenye viungo pungufu au zaidi.

  • Dawa ya mseto ya malaria au ALU; dawa hii ni salama kipindi chote cha ujauzito isipokua miezi mitatu ya kwanza ambapo dawa hii huweza kuingilia ukuaji wa maumbile ya kwanza ya mtoto[organogenesis} na kutoa motto asiye na viungo vya kawaida.

  • Metronidazole au fragile; hii dawa ipo kwenye kikundi cha antibayotiki yaani hushambulia bakteria. Dawa hii hutumika mara nyingi kuua minyoo ya amiba na kutibu magonjwa ya mfuko wa uzazi wa mwanamke na ikitumika miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito huingilia mfumo wa utengenezaji wa viungo vya mtoto.

  • Mesoprostol: hii ni dawa ambayo iko kwenye kikundi maarufu cha prostanglandins analogue, hutumika sana kuongeza njia ya mlango wa uzazi kipindi cha kujifungua na pia hutumika kutibu madonda ya tumboni hivyo matumizi ya dawa hii kipindi cha ujauzito yana madhara makubwa mno ikiwemo kutoa mimba kabisa.

  • Aspirin: hii ni dawa ya maumivu ambayo humezwa mara kwa mara na hupatikana kirahisi tu, lakini dawa hii ina uwezo wa kusababisha kuvuja kwa damu nyingi hasa mama akipata matatizo flani ya uzazi kama placenta previa. Sio dawa nzuri sana kipindi cha ujauzito.

  • Praziquantel: hii ni dawa inayotumika kutibu minyoo flani inayopatikana kwenye sehemu za maji yaliyotuama, ni hatari sana kwa wamama wajawazito kwani huiingilia mfumo wa ukuaji wa mtoto.

  • Furesamide: hii ni dawa ambayo inapatikana kwenye kikundi cha diuretic.. mara nyingi hutumika kushusha ongezeko la maji nje ya mfumo husika wa damu [oedema] na kutibu presha kubwa ya damu. Sio dawa nzuri kwa akina mama wajawazito kwani wajawazito hua na presha ya chini kidogo hivyo huweza kuishusha chini kabisa[intravascular volume depletion].
Image result for MADAWA HATARI KWA MJAMZITO
Mwisho: usitumie dawa yeyote kipindi cha ujauzito bila ushauri wa daktari kwani ni hatari sana kwa maisha yako na mtoto wako kwa ujumla.

1. Huondoa sumu mwilini haraka sana
2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi
3. Kuna viua vijasumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi
4. Huondoa uvimbe mwilini
5. Huondoa msongamano mapafuni
6. Tangawizi inayo ‘zingibain’ ambayo huua vimelea mbalimbali vya magonjwa na mayai yake
7. Huondoa maumivu ya koo
8. Huua virusi wa homa
9. Huondoa maumivu mbalimbali mwilini
10. Huondoa homa hata homa ya baridi (chills)
11. Hutibu saratani ya tezi dume. Tangawizi huua kimeng’enya ambacho ni chakula cha seli za kansa ya tezi dume kiitwacho ‘5-LO enzymes’ na seli hizo za kansa hufa ndani ya masaa mawili au manne bila hicho kimeng’enya.
12. Tangawizi ina kiinilishe mhimu sana ambacho huzuia kuongezeka kwa seli za kansa ya kongosho kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘gingerol”
13. Hutibu kansa zinazoweza kusababishwa na kupata choo kigumu muda mrefu (constipation-r
elated cancer)
14. Ni dawa nzuri kwa kansa ya kwenye damu (leukemia)
15. Ni dawa nzuri dhidi ya kansa ya mapafu (lung cancer)
16. Huzuia kujizalisha kwa bakteria aitwaye ‘Helicobacter pylori’, bakteria huyu ndiye husababisha vidonda vya tumbo mwilini, pia hutibu kiungulia, na kanza mbalimbali za tumbo
17. Ni msaada sana katika kuzuia na kutibu kansa ya titi
18. Hutibu kanza za kwenye kizazi na kanza za kwenye mirija ya uzazi
19. Huongeza msukumo wa damu
20. Husaidia kuzuia shambulio la moyo
21. Huzuia damu kuganda
22. Hushusha kolesto
23. Husafisha damu
24. Husaidia watu wenye kukakamaa kwa mishipa
25. Hutibu shinikizo la juu la damu
26. Husafisha utumbo mpana
27. Hupunguza mishtuko kwenye utumbo mpana na tumbo kuunguruma
28. Huondoa GESI TUMBONI KIRAHISI ZAIDI
29. Husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula
30. Dawa nzuri ya kuondoa uchovu
31. Husaidia kuzuia kutapika. Husaidia hata wale wanaosafiri baharini wasipatwe na kichefuchefu
32. Husaidia kuondoa maumivu kutokana na mkao mmoja wa mrefu ama kusimama au kukaa
33. Husaidia uzalishwaji wa juisi vimeng’enya kwa ajili ya kumeng’enya chakula
34. Husaidia kuzuia kuharisha
35. Husaidia mfumo wa upumuaji na kutuliza dalili za pumu
36. Hutibu tatizo la miguu kuwaka moto
37. Hutibu homa ya kichwa
38. Hutibu maumivu ya tumbo wakati wa hedhi
39. Hutibu homa za asubuhi hata kwa mama mjamzito
40. Husaidia kupunguza homa ya baridi yabisi (helps reduce inflammation of arthritis)
41. Huimarisha afya ya figo
42. Husaidia kupunguza uchovu unaotokana na matibabu yaliyopita ya mionzi
43. Ina madini ya potassium ya kutosha
44. Ina madini ya manganese ambayo ni mhimu katika kuuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali, hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita
45. Ina kitu kinaitwa ‘silicon’ ambacho chenyewe kazi yake hasa ni kuongeza afya ya ngozi, nywele, meno na kucha
46. Husaidia umeng’enywaji wa madini ya calcium
47. Pia ina vitamini A, C, E, B-complex, chuma, zinki , magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta-carotene
48. Hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita
BLEND KAMA UNAVYO TENGENEZA JUICE YA KAWAIDA KISHA KUNYWA GLASS MOJA KWA SIKU.
AU UNAWEZA KUJENGA MAZOEA YA KUTAFUNA VIPANDE KADHAA KILA SIKU ASUBUHI KABLA HUJALA KITU
Tafadhari share kwa ajili ya wengine

Saturday, October 7, 2017

UMUHIMU WA KUNYONYESHA MAZIWA YA MAMA Kunyonyesha maziwa ya mama kunampa Mama Pamoja na Mtoto faida nyingi.

Faida kwa mtoto:

• Humpatia virutubisho (viini lishe) vyote anavyohitaji kwa uwiano ulio sahihi
kwa ukuaji na maendeleo yake;

• Humpatia kinga dhidi ya maradhi mbalimbali kama kuharisha, magonjwa ya
njia ya hewa na masikio;

• Humwezesha mtoto kukua kimwili na kiakili kikamilifu;

• Huleta uhusiano mzuri na wa karibu kati ya mama na mtoto;

• Watoto walionyonya maziwa ya mama huwa na mwenendo mzuri pamoja na
akili ukilinganisha na wale wasionyonya maziwa ya mama.

• Maziwa ya mama humeng’enywa (huyeyushwa) kwa urahisi tumboni mwa
mtoto na hivyo kutumiwa na mwili kwa ufanisi.

Kunyonyesha kunasaidia kumkinga

mtoto na magonjwa mbalimbali

Faida kwa mama:

Huchangia katika kulinda afya ya mama kwa njia mbalimbali kama zifuatazo:

• Mama anaponyonyesha mara baada ya kujifungua husaidia tumbo la uzazi
kurudi katika hali ya kawaida mapema. Na pia husaidia kupunguza damu kutoka
hivyo kuzuia upungufu wa wekundu wa damu (upungufu wa damu);

• Hupunguza uwezekano wa kupata ujauzito katika miezi sita ya mwanzo kama
mama atamnyonyesha mtoto maziwa yake tu mara nyingi kwa siku na pia
kama hajapata hedhi;

• Hupunguza uwezekano wa kupata saratani ya mfuko wa uzazi, na matiti;

• Hujenga uhusiano wa karibu kati ya mama na mtoto; na

Unyonyeshaji bora wa Maziwa ya Mama 5

Kunyonyesha kunasaidia kumkinga

mtoto na magonjwa mbalimbali

• Iwapo mama aliongeza uzito mwingi wakati wa mimba, kunyonyesha husaidia
kumrudishia mama umbile lake la kawaida.
Faida nyingine za maziwa ya mama:
• Ni safi na salama, hupatikana muda wote katika joto sahihi kwa mtoto na
hayahitaji matayarisho;

• Hayaharibiki ndani ya titi na hata yakikamuliwa huweza kukaa saa 8 katika
joto la kawaida bila kuharibika, na saa 72 kwenye jokofu;

• Gharama yake ni ndogo ukilinganisha na maziwa mbadala;

• Huokoa fedha za kigeni ambazo zingenunulia maziwa mbadala na madawa;

• Huokoa muda wa mama na fedha za familia ambazo zingenunua maziwa
mbadala au kulipia matibabu;

• Hayaleti matatizo ya mzio (“allergies”) kama pumu (asthma ) na magonjwa ya
ngozi;
• Maziwa ya mama hutunza mazingira, kwani hayaachi mabaki kama makopo na
chupa ambavyo hutumika kwa maziwa mbadala.

Mtoto aanze kunyonyeshwa maziwa ya mama yake mara tu
anapozaliwa

Friday, September 29, 2017

 
Image result for JE NI SAHIHI MAMA MJAMZITO KUFANYA MAPENZI
kuna watu wamekua wakiuliza mara kwa mara kama inaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka umri gani wa mimba au ni sahihi kufanya tendo la ndoa kipindi cha ujauzito? maswali yalikua mengi sana hivyo leo nimeamua nijibu maswali hayo na makala hii.
mwanamke akiwa na mimba anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa hata kama anatarajia kuzaa kesho yake, hakuna tatizo lolote linalomzuia kufanya hivyo, baadhi ya wanawake wamekua wazito sana kufanya hivyo kwa kua na sababu mbalimbali za kujitetea bila kujua kwamba wanazikosa faida hizi ambazo ni muhumu kiafya.faida zenyewe ni kama zifuatazo

husaidia uchungu mzuri na kupona mapema; kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa huambatana na kubana kwa misuli ya nyonga hii husaidia kuweka imara misuli ya nyonga ambayo ni muhimu sana wakati wa kusukuma mtoto na baada ya kuzaa kwani misuli hii ikiwa legevu mwanamke huweza kushindwa kuzaa kwa njia ya kawaida na hata baada ya kuzaa huweza kushindwa kuzuia mkojo usitoke wenyewe au kuvuja damu kwa muda mrefu.
hupunguza kwenda ovyo kukojoa au kujikojolea; wakati wa ujauzito mtoto anapozidi kua mkubwa anazidi kukandamiza kibovu cha mkojo, hii humfanya mama aende chooni kukojoa mara kwa mara na wakati mwingine hata akipiga chafya au kukohoa basi mkojo unaweza kutoka wenyewe. tendo la ndoa huibana misuli ya nyonga na kuzuia hali hii.

huzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba; tafiti zinaonyesha kwamba aina ya protini inayopatikana kwenye mbegu za mwanaume huongeza kinga ya mwili na kuzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba ambacho kinaua wanawake wengi sana.

hutibu tatizo la kufika kileleni kwa shida; kipindi cha ujauzito chuchu za mwanamke na kinembe chake huvimba na kuongezeka hisia mara dufu huku kiwango cha homoni za oestrogen kikiwa juu sana, hii humfanya kufika kileleni kirahisi sana kuliko mwanzoni.

huwapa uwezo wa kujiamini; kipindi cha ujauzito mwanamke hua anapata hofu sana na kutojiamini na mwili wake, hua na wasiwasi kwamba mwili wake unaharibika hivyo kitendo cha mwanaume wake kuendelea kushiriki naye tendo la ndoa humpa kujiamini kwamba mwili wake bado uko kwenye hali nzuri na anapendwa.

hupunguza msongo wa mawazo; kipindi cha ujauzito wanawake wengi huwaza sana kuhusu kesho yao...je swala la uchumi litakuaje? mwili wangu utakuaje? je ntapata jinsia nayotegemea? na kadhalika.. tendo la ndoa hutoa homoni ya upendo kwa jina la oxytocin, homoni hii hupunguza mawazo na kumpa amani mjamzito.

huongeza upendo na mshikamano  kati ya wapenzi; katika hali ya kawaida wanandoa wakikwazana wanaweza wakapatana kwa kushiriki tendo la ndoa tu, amani na upendo kipindi hiki ni muhimu sana kwani kuna mtoto anakuja ambaye anatakiwa kuzaliwa huku baba na mama wakiwa wanapatana.

hukuandaa na uchungu; ukishiriki ndoa wakati wa tarehe zilizokadiriwa zimefika unapata homoni moja kutoka kwenye mbegu za  mwanaume kwa jina la prostglandin, homoni hii huivisha mlango wa uzazi na kuanza kufunguka taratibu kujiandaa na uchungu.

hutibu tatizo la kukosa usingizi; wanawake wengi wajawazito hua na dalili mbalimbali za maumivu na kuumwa sehemu tofauti za mwili na msongo wa mawazo, hii huweza kuwakosesha usingizi kabisa..tendo la ndoa huweza kuwapa usingizi mzuri.
hupunguza presha ya damu; kipindi cha tendo la ndoa presha ya damu hushuka kwenye kiwango kizuri sana, hii ni muhimu sana kwa wanawake wenye hatari ya kupata kifafa cha mimba kama wanene sana, wenye kisukari au wenye historia za ugonjwa wa presha kwenye koo zao.
mwisho; hakikisha unatumia staili za tendo la ndoa ambazo hazimuumizi mtoto na mama yaani hakikisha haulilalii tumbo hasa mimba ikiwa kubwa, kuna staili muhimu kipindi hiki kama kuangalia upande mmoja, mwanamke kuja juu, au mwanamke kuinama
 Image result for HATUA ZA UKUAJI WA MTOTO
wakati wa kuzaliwa;mtoto hupungua uzito kwa 5% mpaka 10% ndani ya siku saba mpaka kumi za kuzaliwa, baadae mtoto huongezeka kilo mbili kila mwaka mpaka atakapofikisha miaka mitano, mtoto huzaliwa na urefu wa sentimita 50, baada ya mwaka mmoja hufikisha sentimita 75 na na baada ya miaka minne hufikisha urefu wa sentimita 100.
mtoto huzaliwa na kichwa chenye mzunguko au diameter au mzunguko  wa sentimita 35 na kuongezeka sentimita moja kila mwezi na baada ya miezi 12 kichwa hufikisha sentimita 46

wiki ya sita; katika umri huu mtoto huanza kutabasamu bila kuongea chochote.

mwezi wa pili; mtoto huanza kukunja na kunyoosha mikono huku akivuta nguo zake na za mtu anayembeba.

mwezi wa nne; kipindi hiki mtoto huanza kushika vitu na kuviweka mdomoni na kuanza kugeuka pale anaposikia sauti ya mtu inaita na kuweza kutumia shingo lake japokua wakati mwingine huweza kushika shingo akiwa na miezi mitatu tu.

mwezi wa sita; kipindi hiki mtoto huota meno, huanza kutambaa, huanza kukaa mwenyewe na hupata wasiwasi akimuona mtu ambaye hamfahamu.

mwezi wa tisa; mtoto huanza kusimama, kuita majina kama dada, mama, kaka na kuanza kucheza michezo ya kitoto.

mwezi wa 12; mtoto huanza kutembea kwa sapoti ya kushikwa au kutumia vifaa maalumu vya kusukuma, huanza kuongeza maneno zaidi ya kaka na dada na pia huweza kushika kikombe na kunywa mwenyewe.

mwezi wa 15; mtoto huanza kutembea mwenyewe, huweza kuchora mstari na kuonyesha kitu anachokihitaji kwa kidole.

mwezi wa 18; mtoto huweza kupanda ngazi, huongeza idadi ya maneno na hufuata akiagizwa kufanya au kutofanya kitu fulani, hapa huanza kutumia kijiko na kujishika sehemu za mwili wake.

miaka miwili; hapa mtoto huweza kukimbia na kupiga mpira, huweza kuvua nguo na kuanza kutamka maneno kama mimi, wewe yule na kadhalika.

miaka mitatu; hapa mtoto anazidi kua mkubwa na kuanza kusimama kwa mguu mmoja, kukimbia zaidi, kujua jinsia na umri wake, huweza kuvaa na kuvua nguo lakini hawezi kufunga vifungo, anaweza kuhesabu moja mpaka kumi kama akifundishwa, anaweza kuruka na kuchora duara.

miaka minne; mtoto anaweza kusimulia kitu kilichomtokea, kutumia choo na kufunga vifungo, huweza kucheza michezo mingi zaidi, huweza kuruka kwa mguu moja bila kuanguka.

miaka mitano; mtoto anaweza kuzitambua rangi nne za msingi, anaweza kuendesha baiskeli, anaongea kama watu wengine bila kuchanganya wakati uliopo na ujao.

mwisho; utaratibu wa kwenda kliniki kwa muda wa miaka mitano uliwekwa ili kuhakikisha mtoto anafuatiliwa na hachelewi kukua na kama kuna tatizo lolote basi lifanyiwe kazi kwa wakati hivyo ni muhimu kuendelea kwenda kliniki hata kama unaona mtoto amekua.
hatua hizo za ukuaji zinatofautiana kulingana na mataifa mbalimbali lakini mtoto wako akiwahi kufanya vitu sio dhambi ila ukiona anachelewa kupita kiasi basi ni dalili mbaya ya ukuaji na kliniki watakwambia.

 Image result for KUZOROTA AFYA YA MTOTO

Kuna imani imekuwa ikijitokeza kwamba kufanya mapenzi kipindi wakati mtoto angali ananyonya ndio hupelekea hali ya mtoto kuwa mbaya huku ikifahamika kama KUBEMENDA lakini katika hali halisi hii si kweli kabisa kwani kuzorota kwa afaya ya mtoto husababishwa na mambo yafuatayo.

  • Kukosa maziwa ya mama ya kutosha

  • Mtoto kushindwa kunyonya vizuri

  • Kuanzishiwa vyakula vya ziada mapema, kabla mtoto hajafikisha miezi 6 au vyakula visivyo na viritubisho vya kutosha.

  • Homa, nimonia na maambukizi ya mfumo wa mkojo (uti) za mara kwa mara.

  • Maambukizi ya magonjwa kama virusi vya ukimwi (vvu) au kifua kikuu.

  • Matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo (congenital heart diseases).

    KAMA MZAZI IANAKUPASA KUMJUA NA KUMCHUNGUZA MTOTO WAKO KILA WAKATI ILI KUWEZA KUBAINI TATIZO LIKO SEHEMU IPI NA UWEZE KUMTIBIA MAPEMA.

Tuesday, September 5, 2017


Image result for lishe bora ya mtoto
hakuna mzazi asiyependa kumuona mtoto wake katika hali nzuri na yenye afya, je unadhani ni lishe ipi inafaa kwa mwanao!?

1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote ameona chakula flani kime work kwake basi tu share nasi kujaribu kama kitapendwa pia....

2)tujuzane trick gani unatumia wakati wa kumlisha mtoto binafsi mimi huwa namfunga kwenye kiti chake alafu nampa kijiko au kipaja cha kuku sasa wakati anafungua mdomo kutafuna alichokikamata mie namuwahi kupitisha kijiko cha chakula hii inasaidia sana na tricks nyengine tutazidi kujuzana...

Karibuni wote tujadili au tupia recipe zako.

Lishe (1) - UJI WA OATS NA NDIZI/APPLE


Mahitaji

Oats kiasi

Apple 1 au ndizi ya kuwiva...

Maziwa...

Sukari (sio lazima)...

Namna ya kutaarisha

Chemsha maji

Weka oats acha zichemke hadi kuwiva

Ponda ponda ndizi vizuri weka maziwa kidogo ipondeke vizuri....

Mimina kwenye oats alafu weka na maziwa acha ichemke kidogo kwa dakika 3

Epua mlishe mtoto.....

Image result for lishe bora ya mtoto

Lishe (3) - WALI WA YAI

Mahitaji

Yai 1....tumia kiini tu

Siagi kidogo

Mchele....

Namna ya kutaarisha...

Pika wali kama wa kawaida ila weka maji mengi uwe laini bwabwa wengine wanaita bondo

Ukikaribia kuwiva weka yai ulolivunja koroga haraka haraka uchanganyike vizuri

Weka siagi na chumvi kidogo ukipenda....

Epua mlishe mtoto....


Lishe (3) - KAROTI NA KUKU


Mahitaji

Karoti

Kuku kiasi


Namna ya kutaarisha

Chemsha kuku hadi kuwiva iwe na supu kidogo

Weka karoti na subiria kuwiva...

Toa kuku pembeni alafu mchambue mifupa tupa

Weka katika blenda kuku na katoti na supu yako saga

Tayari kwa kumlisha mtoto

Ukipendeza waweza weka na viazi
Image result for lishe bora ya mtoto


#jamiiforum
Image result for madhara ya fangasi kwa mjamzito
Maambukizi  ya fangasi kwa mama mjamzito hutokea kutokana na kubadilika
kwa homoni mwilini ikiambatana na upungufu wa kinga mwilini huku
ikielezwa kuwa si kila mjamzito ana uwezekano wa kupata maambukizi.

Matumizi ya vidonge vya kupanga uzazi vimetajwa kuwa kisababishi kimoja
wapo kinachoweza kumfanya mama mjamzito apate fangasi hasa wa aina ya
Candida albicans.

Wakinamama wajawazito wanaoweza kupata maambukizi ya fangasi ni wale
wenye tabia ya kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri
kama nguo za kuogelea (swim wear), nguo za ndani zilizotengenezwa kwa
kitambaa aina ya nailon au zinazobana sana.

Akizungumza na mwandishi wa Hivisasa Afisa matibabu katika zahanati ya
Kigogo Dokta Ambakisye Mwalusamba ameeleza kuwa licha ya matumizi ya
nguo au mavazi yanayoleta joto lakini pia mtindo wa kujamiiana kwa
kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi vyenye
glycerin wakati wa tendo la ndoa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
maambukizi ya maradhi haya.

Aidha ametaja namna muathirika wa maradhi hayo anavyotakiwa kupata
vipimo ni pamoja na kumueleza daktari kumfahamisha mgonjwa aina ya
kipimo, lengo lake na jinsi kitakavyofanyika ili kumuandaa kisaikolojia
huku kabla ya kumfanyia vipimo vya uchunguzi wa uke ambavyo kitaalamu
huitwa Per Vaginal Examination (PV exam) kuona kama kuna uvimbe wowote
ndani ya uke au kama ana maumivu wakati wa kujamiiana hali
Itakayoashiria wazi kuwako kwa aina fulani ya fangasi katika sehemu hizo.

Hata hivyo Daktari anaweza kuchukua kipimo na kuotesha kwenye mahabala
ili kuangalia aina ya uoto huo kama ni wa fangasi aina ya Candida
albicans, au atafanya kipimo cha mkojo (Urinalysis) na cha ugonjwa wa
kisukari, HIV/AIDS, ugonjwa wa  kuvimba tezi la koo (goiter) na kadhalika.

Amefafanua kuwa Dokta ataangalia kama kuna uchafu wowote unaotoka, wingi
wake, rangi yake, harufu yake, uzito wake na aina ya uchafu unaotoka
kama ni sahihi kutokana huku akilinganisha na  maelezo ya mgonjwa.

Jinsi ya kujikinga na Fangasi

– kutovaa nguo za kubana ambazo zitapelekea kusababisha joto ukeni   na
kuacha majimaji  yatakayosababisha fangasi,

– Mama huyo anashauriwa kujifuta na kujikausha vizuri katika sehemu za
siri pindi anapotoaka      kuoga au kujisaidia kutoka kwamba pindi
atakapokuwa katika kipindi cha ujauzito hutoka na jasho mara kwa mara na
kubanwa na haja ndogo.

– Kuacha tabia ya kuvaliana nguo au kuazima nguo za mtu mwingine  huenda
 ikawa ana ugonjwa wa fangasi.
Utamaduni wa Tanzania unapendekeza wanawake kuvaa nguo kubwa, zilizopwaya wakati wa ujauzito. Kama vile hawana haja ya kupendeza wakiwa wajawazito. Bahati nzuri, kuna maduka mengi zenye mavazi mazuri za wakati wa ujauzito.
Image result for mavazi ya mama mjamzito
Ila bado kuna wanawake wengi wanaoamua kutojali muonekano wao wakiwa wajawazito. Sasa, kwa wao, vidokezo vifuatayo vitakusaidia kuvaa ukiwa mjauzito.

1. Kubali umbo lako
Hamna haja ya kuficha ujauzito wako. Ila hatusema kwamba uvae blauzi inayobana na kimini (ila, unaweza kuvaa hivyo ukipenda). Tunachopendekeza hapa ni kuvaa nguo zinazotosha umbo lako.Tumbo lako likianza kujitokeza, nunua nguo kama gauni, jinzi na topu zinazo ruhusu hewa kupita; hizi zitakuwezesha kuonyesha figure yako kwa kistaarabu.

2. Usibadilishe mtindo wako wa kawaida
Kwa kuwa we ni mjazmzito haimaanisha kwamba inabidi ubadilishe mtindo wako wa kipekee.
Kwa hiyo, kama ulikuwa unapenda gauni, endelea kuvaa gauni. Hakikisha inatosha umbo lako tu.

3. Tumia vifaa vya mitindo
Scafu, bangili, ereni n.k zitasaidia kuboresha vazi lako kwa ujumla na zitakusaidia kujiamini pia. Kwa mfano, kama unawasiwasi na tumbo lako lilivyojitokeza, vaa mkufu au ereni safi zitakazo fanya watu waangalie sura badala ya tumbo yako.

4. Nunua Jinzi safi kwa ajili ya ujauzito
Nunua jinzi zenye uwezo wa kupanuka ndio zitakazokufaa. Zinaweza zikawa za kubana au zenye nafasi zaidi, cha muhimu nikwambai unajisikia vizuri ukizivaa.

5. Nunua gauni ya kufunga (Wrap Dress)
Wrap Dress zinafaa kwa umbo yoyote ile na zinapendeza sana! Pia ni rahisi kuzivaa na kutembea ndani yao ukiwa umezivaa.
 
6. Nunua nguo zenye rangi kali
Rangi kali kama njano na rangi ya machungwa (orange) zinaonyesha ile mwanga asili ambao wajawazito huwa wanao. Kwa hiyo, kuvaa gauni yenye rangi kali inaweza ikampa mjamzito mng’ao wa kirembo.

Onekana vizuri zaidi ya unavyojisikia
Kuwa mjamzito ni wakati muhimu katika maisha ya mwanamke na kwa kuwa hutajisikia vizuri kila siku ya ujazito wako, unaweza kuendelea kupendeza na kutafuta nguo zitakazoipendza mwili wako.
Image result for mavazi ya mama mjamzito

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR