hakuna mzazi asiyependa kumuona mtoto wake katika hali nzuri na yenye afya, je unadhani ni lishe ipi inafaa kwa mwanao!?
1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote ameona chakula flani kime work kwake basi tu share nasi kujaribu kama kitapendwa pia....
2)tujuzane trick gani unatumia wakati wa kumlisha mtoto binafsi mimi huwa namfunga kwenye kiti chake alafu nampa kijiko au kipaja cha kuku sasa wakati anafungua mdomo kutafuna alichokikamata mie namuwahi kupitisha kijiko cha chakula hii inasaidia sana na tricks nyengine tutazidi kujuzana...
Karibuni wote tujadili au tupia recipe zako.
Lishe (1) - UJI WA OATS NA NDIZI/APPLE
Mahitaji
Oats kiasi
Apple 1 au ndizi ya kuwiva...
Maziwa...
Sukari (sio lazima)...
Namna ya kutaarisha
Chemsha maji
Weka oats acha zichemke hadi kuwiva
Ponda ponda ndizi vizuri weka maziwa kidogo ipondeke vizuri....
Mimina kwenye oats alafu weka na maziwa acha ichemke kidogo kwa dakika 3
Epua mlishe mtoto.....
Lishe (3) - WALI WA YAI
Mahitaji
Yai 1....tumia kiini tu
Siagi kidogo
Mchele....
Namna ya kutaarisha...
Pika wali kama wa kawaida ila weka maji mengi uwe laini bwabwa wengine wanaita bondo
Ukikaribia kuwiva weka yai ulolivunja koroga haraka haraka uchanganyike vizuri
Weka siagi na chumvi kidogo ukipenda....
Epua mlishe mtoto....
Lishe (3) - KAROTI NA KUKU
Mahitaji
Karoti
Kuku kiasi
Namna ya kutaarisha
Chemsha kuku hadi kuwiva iwe na supu kidogo
Weka karoti na subiria kuwiva...
Toa kuku pembeni alafu mchambue mifupa tupa
Weka katika blenda kuku na katoti na supu yako saga
Tayari kwa kumlisha mtoto
Ukipendeza waweza weka na viazi
#jamiiforum
0 comments:
Post a Comment