Tuesday, September 5, 2017


Image result for lishe bora ya mtoto
hakuna mzazi asiyependa kumuona mtoto wake katika hali nzuri na yenye afya, je unadhani ni lishe ipi inafaa kwa mwanao!?

1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote ameona chakula flani kime work kwake basi tu share nasi kujaribu kama kitapendwa pia....

2)tujuzane trick gani unatumia wakati wa kumlisha mtoto binafsi mimi huwa namfunga kwenye kiti chake alafu nampa kijiko au kipaja cha kuku sasa wakati anafungua mdomo kutafuna alichokikamata mie namuwahi kupitisha kijiko cha chakula hii inasaidia sana na tricks nyengine tutazidi kujuzana...

Karibuni wote tujadili au tupia recipe zako.

Lishe (1) - UJI WA OATS NA NDIZI/APPLE


Mahitaji

Oats kiasi

Apple 1 au ndizi ya kuwiva...

Maziwa...

Sukari (sio lazima)...

Namna ya kutaarisha

Chemsha maji

Weka oats acha zichemke hadi kuwiva

Ponda ponda ndizi vizuri weka maziwa kidogo ipondeke vizuri....

Mimina kwenye oats alafu weka na maziwa acha ichemke kidogo kwa dakika 3

Epua mlishe mtoto.....

Image result for lishe bora ya mtoto

Lishe (3) - WALI WA YAI

Mahitaji

Yai 1....tumia kiini tu

Siagi kidogo

Mchele....

Namna ya kutaarisha...

Pika wali kama wa kawaida ila weka maji mengi uwe laini bwabwa wengine wanaita bondo

Ukikaribia kuwiva weka yai ulolivunja koroga haraka haraka uchanganyike vizuri

Weka siagi na chumvi kidogo ukipenda....

Epua mlishe mtoto....


Lishe (3) - KAROTI NA KUKU


Mahitaji

Karoti

Kuku kiasi


Namna ya kutaarisha

Chemsha kuku hadi kuwiva iwe na supu kidogo

Weka karoti na subiria kuwiva...

Toa kuku pembeni alafu mchambue mifupa tupa

Weka katika blenda kuku na katoti na supu yako saga

Tayari kwa kumlisha mtoto

Ukipendeza waweza weka na viazi
Image result for lishe bora ya mtoto


#jamiiforum

Related Posts:

  • MAMBO MUHIMU KUHUSU UNYONYESHAJI WA WATOTO.Unyonyeshaji wa watoto ni njia iliyo thabiti kabisa kuhakikisha mtoto anakua akiwa mwenye afya njema na hupunguza vifo kwa watoto kwa kiasi kikubwa. Kama mtoto atanyonyeshwa  saa moja baada ya kuzaliwa, na kuendelea… Read More
  • MLO ULIO BORA KWA MTOTO Huwa ni furaha kubwa katika familia mtoto anapozaliwa, na hata katika tamaduni fulani fulani sherehe kubwa hufanyika kumkaribisha mwanafamilia mpya aliyezaliwa. Lakini pamoja na familia kuwa katika hali ya furaha, wazazi w… Read More
  • LISHE BORA KWA MTOTO WAKO. hakuna mzazi asiyependa kumuona mtoto wake katika hali nzuri na yenye afya, je unadhani ni lishe ipi inafaa kwa mwanao!? 1)kwa wale watoto ambao hawapendi kula au hatujatambua bado nini wanapenda lakini kuna mzazi yeyote a… Read More
  • LISHE YA MTOTO BAADA YA MAZIWA KUANZA Wadau mbalimbali wamekua wakinitumia mails kuniulizia kila kitu kinachohusu kulisha mtoto chakula, kuanzai jinsi ya kumuanzisha, lini aanzishwe hadi apewe nini.Kiukweli nimejitahidi kujibu, sasa naona zinanielemea na wada… Read More

0 comments:

Post a Comment

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR