Thursday, June 29, 2017

Wanawake wanaokula udongo wakiwa wajiwazito wamo katika hatari ya kuwafanya watoto watakowajifungua kutofanya vizuri shuleni.

Utafiti uliofanywa unaonyesha kuwa watoto ambao kina mama wao walikuwa wakitumia udongo hawakomakiniki darasani.

Kwa kawaida wanawake wengi hutumia udongo huo baadhi wakidai kuwa wana upungufu wa madini ila wengi wao huzidisha matumizi yake.

Zaidi ya wazazi 4000 walihusishwa katika utafiti huo lakini ni 1000 tu ambao maoni yao yalitumika kuandaa ripoti ya utafiti huo.

Taasisi hiyo ilikuwa ikifuatilia matokeo ya watoto hao wakiwa shuleni kwa muda wa miaka minne na wakatambua kuwa wale ambao hawakuwa imara darasani mama zao walikuwa na historia ya kutumia udongo wakiwa wamebeba mimba zao.

Watafiti hao wanasema kuwa kutokana na hayo ubongo wa watoto waliozaliwa huchelewa kushika mambo.

Kadhalika utafiti huo unaonyesha kuwa wanawake katika miaka ya ishirini huwa na hamu kubwa kutumia udongo.

Nini maoni yako juu ya matumizi ya udongo kwa wajawazito!?

Related Posts:

  • FAIDA ZA KUNYONYESHA KWA MAMA NA MTOTO.UMUHIMU WA KUNYONYESHA MAZIWA YA MAMA Kunyonyesha maziwa ya mama kunampa Mama Pamoja na Mtoto faida nyingi. Faida kwa mtoto: • Humpatia virutubisho (viini lishe) vyote anavyohitaji kwa uwiano ulio sahihi kwa ukuaji na m… Read More
  • MGONGO WAZI NA VICHWA KUJAA MAJIUgonjwa wa mtoto kuzaliwa na nafasi kwenye uti wa mgongo unaitwa Spina Bifidaugonjwa huu hutokana na upungufu wa vitamin B9 (foliac acid). mama mjamzito hutakiwa kutumia vitamin B9 wakati wa ujauzito au wakati anpopanga kuwa… Read More
  • ZIFAHAMU FAIDA 48 ZA JUICE YA TANGAWIZI.1. Huondoa sumu mwilini haraka sana 2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi 3. Kuna viua vijasumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi 4. Huondoa uvimbe mwilini 5. H… Read More
  •   dawa ambazo jamii yetu huzitumia mara kwa mara kujitibu magonjwa mbalimbali na hupatikana kirahisi mtaani Lakini  bahati mbaya baadhi ya dawa hizo hazitakiwi kupewa kwa wajawazito kabisa kulingana na madhara mak… Read More
  • REKEBISHA HOMONI UWEZE KUITWA MAMAHomoni zina mchango mkubwa katika afya kwa ujumla katika mwili wa mwanamke hasa linapokuja suala la uzazi. Mara nyingi usawa usio sawa wa homoni husababishwa na mabadiliko katika homoni ya ‘estrogen’. Mabadiliko h… Read More

0 comments:

Post a Comment

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR