Showing posts with label UZAZI. Show all posts
Showing posts with label UZAZI. Show all posts

Saturday, December 23, 2017

Homoni zina mchango mkubwa katika afya kwa ujumla katika mwili wa mwanamke hasa linapokuja suala la uzazi. Mara nyingi usawa usio sawa wa homoni husababishwa na mabadiliko katika homoni ya ‘estrogen’.

Mabadiliko haya mara nyingi hutokea wakati wa kuvunja ungo, wakati wa hedhi, wakati wa ujauzito na wakati wa ukomo wa hedhi (menopause).

Vitu vingine vinavyopelekea mabadiliko ya homoni ni pamoja na kuongezeka umri, lishe duni, kutokujishughulisha na mazoezi, kupungua kwa ogani ya adreno, mfadhaiko au stress, kukosa usingizi, dawa za uzazi wa mpango, sumu na kemikali mbalimbali nk.
Wanawake wengi hukata tamaa ya kupata mtoto kwa kudhani Ni wagumba kumbe wakati mwingine  huwa Ni tatizo LA homoni imbalance .
sasa utajuaje unahomoni imbalance!? Na je, ufanyeje!?

Dalili zitakazokuonyesha homoni zako hazipo sawa ni pamoja na:

1. Kuwa na tabia ya hamaki (kukosa utulivu)
2. Uchovu sugu
3. Kuongezeka uzito
4. Kupungua kwa nywele
5. Maumivu ya kichwa ya mara kwa mara
6. Kukosa hamu ya tendo la ndoa
7. Chunusi
8. Kuwa na hamu na vyakula au vinywaji vya viwandani kila mara
9. Kushindwa kushika ujauzito
10. Kutokujisikia vizuri kila mara bila sababu maalumu
11. Kukosa usingizi
12. Hasira zisizo na sababu maalumu nk

Zipo dawa za asili zinazoweza kukusaidia kurekebisha na hatimaye kuweka sawa usawa wa homoni mwilini mwako.

Ni mhimu uonane na daktari kabla kwa uchunguzi, vipimo na ushauri zaidi kabla ya kuamua kutumia hivi vinavyopendekezwa kwenye makala hii hasa kama una matatizo kama ya uvimbe katika kizazi, saratani ya matiti, saratani ya kizazi au una saratani katika mirija ya uzazi.

Njia mbadala 6 za kurekebisha homoni zako na hatimaye upate ujauzito:

1. TUMIA OMEGA 3 KILA SIKU

Asidi mafuta yenye Omega-3 yana umhimu mkubwa katika kuweka sawa homoni zako.

Kwa wanawake yana umhimu mkubwa kwani husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi usiosawa na kupunguza dalili za kukoma kwa hedhi (menopausal symptoms). Omega-3 husaidia kuondoa sumu mwilini na vivimbe sehemu mbalimbali za mwili.

• Vitu vyenye omega 3 kwa wingi ni pamoja na mafuta ya samaki (yasiyo na mercury), walnuts, maharage ya soya, mafuta ya nazi, mafuta ya zeituni, mafuta ya mawese na mbegu za maboga. Tumia hivi vitu kila siku katika kuishi kwako ili kuweka sawa homoni zako.

2. VITAMINI D

Vitamini D ni mhimu kwa ajili ya tezi ya pituitari (pituitary gland) iweze kufanya kazi zake vizuri na ni tezi inayotengeneza homoni zingine nyingi mhimu.

Vitamini D pia husaidia kuondoa dalili zinazohusiana na usawa mdogo wa homoni ya ‘estrogen’. Vitamini D pia ina uhusiano na kiwango cha njaa ulichonacho na uzito pia.

Upungufu wa vitamini D unaweza pia kupelekea utolewaji usiosawa wa homoni nyingine ijulikanayo kama ‘parathyroid’.

• Tembea juani wakati wa jua kali dakika 20 hadi 30 kila siku huku ukiwa wazi sehemu kubwa ya mwili wako.

• Kula vyakula kama mafuta ya samaki, maziwa na mayai ya kuku wa kienyeji kila siku.

3. JISHUGHULISHE NA MAZOEZI YA VIUNGO

Kujishughulisha na mazoezi ya viungo ndiyo njia rahisi ya kurekebisha homoni zako kwani mazoezi yanahusika katika uzalishaji wa hizo homoni. Mazoezi huipunguza nguvu homoni inayohusika na mfadhaiko (stresss) ijulikanayo kwa kitaalamu kama ‘cortisol’.

Hii homoni ya Cortisol huidhibiti homoni nyingine mhimu ijulikanayo kama ‘estrogen’ ambayo kama itazidi basi inaweza kuleta madhara kwa afya yako yote kwa ujumla.

Mazoezi ya mara kwa mara huusaidia ubongo kutoa kemikali ambazo huongeza hali ya kujisikia vizuri (improves your mood). Jambo hili la kupelekea ujisikie vizuri husaidia kuweka sawa homoni zako.

Siyo hilo tu mazoezi yatakusaidia pia kuwa na uzito sahihi kwani uzito uliozidi ni sababu mojawapo inayopelekea homoni zako kutokuwa sawa.

Nusu saa ya mazoezi kwa siku inatosha. Tatizo wanawake wengi hawana habari na kitu kinaitwa mazoezi!

• Nenda kaogelee, katembee kwa miguu lisaa limoja, au kimbia taratibu (jogging) mara 3 mpaka 4 kwa wiki.

4. TUMIA MAFUTA YA NAZI

Mafuta ya nazi yale ya asili yaliyotengenezwa nyumbani bila kupita kiwandani ni dawa nyingine nzuri ya asili ya kurekebisha na kuweka sawa homoni zako. Mafuta haya huiwezesha tezi ya koromeo (thyroid) kufanya kazi zake vizuri.

Mafuta ya nazi pia husaidia kuweka sawa sukari katika damu, huongeza kinga ya mwili, huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kusaidia pia kupunguza uzito. Mafuta haya ni mazuri kwa afya ya moyo wako na hayana kolesto yoyote mbaya.

Kunywa vijiko vikubwa viwili kila siku kwa mwezi mmoja hata miwili au hata mitatu kwa uhakika wa matokeo mazuri zaidi. Unaweza pia kuyaweka kwenye kachumbali. Pia nakushauri kila upikapo wali tumia tui zito la nazi na siyo wali tu hata katika mapishi mengine unaweza kutumia tui la nazi, kazi ni kwako.

5. UWATU PIA HUREKEBISHA HOMONI

Madaktari wengi wa tiba asili duniani hushauri kutumia uwatu (kwa Kiingereza huitwa ‘fenugreeek’) kwa ajili ya kuongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha. Uwatu hutumika pia kama dawa ya asili ya kuongeza ukubwa wa matiti (natural breast enlargement).

Uwatu husaidia umeng’enywaji wa sukari mwilini na hivyo kuwa msaada mkubwa kwa watu wanaosumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na uzito kupita kiasi (obesity).

• Chukua kijiko kikubwa kimoja cha unga wa mbegu za uwatu na uweke ndani ya glasi moja ya maji ya uvuguvugu, koroga vizuri na unywe yote. Fanya hivi kutwa mara 2 kwa mwezi mmoja mpaka miwili.

Unaweza kuongeza asali kidogo kupata radha. Unaweza kutumia pia ndani ya maziwa ya moto hasa kama huna vidonda vya tumbo au kisukari.

6. TUMIA MREHANI (Basil)

Mrehani hutumika pia kama dawa ya asili ya kurekebisha homoni. Huiweka sawa homoni ya ‘cortisol’ ambayo kama itazidi kuwa nyingi inaweza kuleta shida kwenye homoni koromeo (thyroid gland), Mirija ya uzazi na Kongosho. Wakati huo huo mrehani husaidia kuweka sawa akili yako na hivyo huleta hali ya kujisikia vizuri (good mood).

Unaweza kupata Mrehani ukiwa Dar kwenye soko la kisutu au hata kariakoo pia Zanzibar. Ni kiungo mhimu katika mahoteli mengi ya kitalii.

• Tengeneza chai ukitumia majani fresh ya mmea huu na unywe kikombe kimoja kutwa mara 3 kwa miezi miwili hadi mitatu.

MAMBO YA MHIMU KUZINGATIA:

Pamoja na dawa, zingatia haya yafuatayo kwa matokeo mazuri zaidi:

• Kula parachichi 1 kila siku
• Tumia vyakula asili zaidi kuliko vya kwenye makopo na migahawani (fast foods)
• Tumia vyakula vyenye nyuzinyuzi (fiber) nyingi kwenye chakula chako
• Epuka kahawa, chai ya rangi, soda nyeusi na vinywaji vingine vyote vyenye kafeina ndani yake
• Achana na msongo wa mawazo (stress) na upate usingizi wa kutosha kila siku
• Usitumie dawa za uzazi wa mpango kama unahitaji kuweka sawa homoni zako
• Epuka vilevi vyote
• Kunywa maji mengi kila siku lita 2 hadi 3
• Usitumie vyakula vya moto kwenye vyombo vya plastiki

Friday, October 20, 2017

 Image result for MADAWA HATARI KWA MJAMZITO
dawa ambazo jamii yetu huzitumia mara kwa mara kujitibu magonjwa mbalimbali na hupatikana kirahisi mtaani Lakini  bahati mbaya baadhi ya dawa hizo hazitakiwi kupewa kwa wajawazito kabisa kulingana na madhara makubwa yanayoambatana na dawa hizo kwa mtoto aliyepo tumboni.
Zifuatazo ni dawa hizo.

  • Albendazole; hii ni dawa ya minyoo ambayo hutumika mara kwa mara kujitibu lakini ni dawa mbaya sana kwa akina mama wajawazito kwani una uwezo wa kutoa mimba kabisa hivyo mebendazole hutumika kama mbadala.

  • Gentamycin: hii ni dawa ambayo iko kwenye mfumo wa sindano tu, mara nyingi hutumika kutibu magonjwa ya mfumo wa mkojo. Dawa hii huharibu kabisa mishipa ya fahamu kitaalamu kama auditory nerve ambayo hutufanya sisi kusikia. Hivyo matumizi ya dawa hii huweza kusababisha mototo kuzaliwa akiwa hasikii yaani kiziwi.

  • Ciproflaxin; hii ni dawa ambayo hupatikana kwenye mfumo wa vidonge na sindano, mara nyingi hutumika kutibu typhoid, UTI au magonjwa ya njia za mkojo na magonjwa baadhi ya zinaa. Dawa hii huharibu ukuuji wa mifupa ya mtoto na huweza kutoa mtoto asiyetembea mwishoni.

  • Doxycline: hii ni dawa ambayo hupatikana kwa mfumo wa dawa za kumeza kitaaalamu kama capsules, dawa hizi ni antibiyotiki yaani hutumika kuua bakteria wa aina tofauti. Bahati mbaya huweza kuingilia mfumo wa utengenezaji wa mtoto ikitumika miezi mitatu ya mwanzo na kusababisha kuzaliwa na motto mwenye viungo pungufu au zaidi.

  • Dawa ya mseto ya malaria au ALU; dawa hii ni salama kipindi chote cha ujauzito isipokua miezi mitatu ya kwanza ambapo dawa hii huweza kuingilia ukuaji wa maumbile ya kwanza ya mtoto[organogenesis} na kutoa motto asiye na viungo vya kawaida.

  • Metronidazole au fragile; hii dawa ipo kwenye kikundi cha antibayotiki yaani hushambulia bakteria. Dawa hii hutumika mara nyingi kuua minyoo ya amiba na kutibu magonjwa ya mfuko wa uzazi wa mwanamke na ikitumika miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito huingilia mfumo wa utengenezaji wa viungo vya mtoto.

  • Mesoprostol: hii ni dawa ambayo iko kwenye kikundi maarufu cha prostanglandins analogue, hutumika sana kuongeza njia ya mlango wa uzazi kipindi cha kujifungua na pia hutumika kutibu madonda ya tumboni hivyo matumizi ya dawa hii kipindi cha ujauzito yana madhara makubwa mno ikiwemo kutoa mimba kabisa.

  • Aspirin: hii ni dawa ya maumivu ambayo humezwa mara kwa mara na hupatikana kirahisi tu, lakini dawa hii ina uwezo wa kusababisha kuvuja kwa damu nyingi hasa mama akipata matatizo flani ya uzazi kama placenta previa. Sio dawa nzuri sana kipindi cha ujauzito.

  • Praziquantel: hii ni dawa inayotumika kutibu minyoo flani inayopatikana kwenye sehemu za maji yaliyotuama, ni hatari sana kwa wamama wajawazito kwani huiingilia mfumo wa ukuaji wa mtoto.

  • Furesamide: hii ni dawa ambayo inapatikana kwenye kikundi cha diuretic.. mara nyingi hutumika kushusha ongezeko la maji nje ya mfumo husika wa damu [oedema] na kutibu presha kubwa ya damu. Sio dawa nzuri kwa akina mama wajawazito kwani wajawazito hua na presha ya chini kidogo hivyo huweza kuishusha chini kabisa[intravascular volume depletion].
Image result for MADAWA HATARI KWA MJAMZITO
Mwisho: usitumie dawa yeyote kipindi cha ujauzito bila ushauri wa daktari kwani ni hatari sana kwa maisha yako na mtoto wako kwa ujumla.

Friday, September 29, 2017

 
Image result for JE NI SAHIHI MAMA MJAMZITO KUFANYA MAPENZI
kuna watu wamekua wakiuliza mara kwa mara kama inaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka umri gani wa mimba au ni sahihi kufanya tendo la ndoa kipindi cha ujauzito? maswali yalikua mengi sana hivyo leo nimeamua nijibu maswali hayo na makala hii.
mwanamke akiwa na mimba anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa hata kama anatarajia kuzaa kesho yake, hakuna tatizo lolote linalomzuia kufanya hivyo, baadhi ya wanawake wamekua wazito sana kufanya hivyo kwa kua na sababu mbalimbali za kujitetea bila kujua kwamba wanazikosa faida hizi ambazo ni muhumu kiafya.faida zenyewe ni kama zifuatazo

husaidia uchungu mzuri na kupona mapema; kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa huambatana na kubana kwa misuli ya nyonga hii husaidia kuweka imara misuli ya nyonga ambayo ni muhimu sana wakati wa kusukuma mtoto na baada ya kuzaa kwani misuli hii ikiwa legevu mwanamke huweza kushindwa kuzaa kwa njia ya kawaida na hata baada ya kuzaa huweza kushindwa kuzuia mkojo usitoke wenyewe au kuvuja damu kwa muda mrefu.
hupunguza kwenda ovyo kukojoa au kujikojolea; wakati wa ujauzito mtoto anapozidi kua mkubwa anazidi kukandamiza kibovu cha mkojo, hii humfanya mama aende chooni kukojoa mara kwa mara na wakati mwingine hata akipiga chafya au kukohoa basi mkojo unaweza kutoka wenyewe. tendo la ndoa huibana misuli ya nyonga na kuzuia hali hii.

huzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba; tafiti zinaonyesha kwamba aina ya protini inayopatikana kwenye mbegu za mwanaume huongeza kinga ya mwili na kuzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba ambacho kinaua wanawake wengi sana.

hutibu tatizo la kufika kileleni kwa shida; kipindi cha ujauzito chuchu za mwanamke na kinembe chake huvimba na kuongezeka hisia mara dufu huku kiwango cha homoni za oestrogen kikiwa juu sana, hii humfanya kufika kileleni kirahisi sana kuliko mwanzoni.

huwapa uwezo wa kujiamini; kipindi cha ujauzito mwanamke hua anapata hofu sana na kutojiamini na mwili wake, hua na wasiwasi kwamba mwili wake unaharibika hivyo kitendo cha mwanaume wake kuendelea kushiriki naye tendo la ndoa humpa kujiamini kwamba mwili wake bado uko kwenye hali nzuri na anapendwa.

hupunguza msongo wa mawazo; kipindi cha ujauzito wanawake wengi huwaza sana kuhusu kesho yao...je swala la uchumi litakuaje? mwili wangu utakuaje? je ntapata jinsia nayotegemea? na kadhalika.. tendo la ndoa hutoa homoni ya upendo kwa jina la oxytocin, homoni hii hupunguza mawazo na kumpa amani mjamzito.

huongeza upendo na mshikamano  kati ya wapenzi; katika hali ya kawaida wanandoa wakikwazana wanaweza wakapatana kwa kushiriki tendo la ndoa tu, amani na upendo kipindi hiki ni muhimu sana kwani kuna mtoto anakuja ambaye anatakiwa kuzaliwa huku baba na mama wakiwa wanapatana.

hukuandaa na uchungu; ukishiriki ndoa wakati wa tarehe zilizokadiriwa zimefika unapata homoni moja kutoka kwenye mbegu za  mwanaume kwa jina la prostglandin, homoni hii huivisha mlango wa uzazi na kuanza kufunguka taratibu kujiandaa na uchungu.

hutibu tatizo la kukosa usingizi; wanawake wengi wajawazito hua na dalili mbalimbali za maumivu na kuumwa sehemu tofauti za mwili na msongo wa mawazo, hii huweza kuwakosesha usingizi kabisa..tendo la ndoa huweza kuwapa usingizi mzuri.
hupunguza presha ya damu; kipindi cha tendo la ndoa presha ya damu hushuka kwenye kiwango kizuri sana, hii ni muhimu sana kwa wanawake wenye hatari ya kupata kifafa cha mimba kama wanene sana, wenye kisukari au wenye historia za ugonjwa wa presha kwenye koo zao.
mwisho; hakikisha unatumia staili za tendo la ndoa ambazo hazimuumizi mtoto na mama yaani hakikisha haulilalii tumbo hasa mimba ikiwa kubwa, kuna staili muhimu kipindi hiki kama kuangalia upande mmoja, mwanamke kuja juu, au mwanamke kuinama

Tuesday, July 11, 2017

Waweza kuwa mjamzito Na bado ukabaki katika ubora wako, inategemea ni namna Gani unajiweka.

Tazama mwanamama huyu anashiriki mashindano ya mbio huku akiwa Na ujauzito Wa miezi mitano, tena anaonekana 'fit'.

#uzazisalama hutegemea afya bora Na mazoezi.

Tuesday, June 20, 2017


 Kina mama wakionyesha mfano wa kuwanyonyesha watoto wachanga katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya Unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika kitaifa wilayani Mufundi mkoani Iringa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Charles Pallangyo akizundua kitabu maalum cha Mwongozo wa Mafunzo ya Ulishaji wa watoto wachanga na wadogo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya Unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika kitaifa wilayani Mufundi mkoani Iringa Juzi (kushoto) ni kaimu mkurugenzi wa...

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR