Saturday, August 5, 2017

Hivi ni baadi ya vyakula ambavyo mama mjamzito au mwanamke anaejiandaa kubeba ujauzito HARUHUSIWI kuvitumia katika kipindi cha ujauzito.

*Nyama mbichi au iliyopikwa lakini haikuiva vizuri, nyama za aina hii husemekana kuwa na bacteria ambao huwezakusababisha ujauzito kutoka au kuzaa mtoto mwenye ulemavu wa kuzaliwa

*Maziwa ya mgando au maziwa ambayo hayajachemshwa, maziwa ya aina hii husemekana kuwa na bacteria ambao wanaweza hatarisha maendeleo ya ujauzito

*Vinywaji vyenye caffeine kama vile kahawa, chai, coca cola na vingine vya asili hiyoMayai mabichi, husemekana kuwa na bacteria wanaoweza kuhatarisha maendeleo ya ujauzito.

*Samaki wabichi wa maji chumvi au samaki waliovuliwa kwa kutumia sumu.

*Vyakula laini na vyenye sukari nyingi kama soft cheeses, cake, chocolate n.k.

*Unywaji wa pombe

*Kula mboga za majani au matunda bila kuyaosha

*Ulaji wa maini
Katika kipindi cha ujauzito au katika maandalizi ya kubeba ujauzito mwanamke anatakiwa kula vyakula vya aina mbalimbali vilivyoandaliwa vizuri na kupikwa vikaiva inavyotakiwa, ulaji wa vyakula mbalimbali katika makundi ya vyakula kabla ya ujauzito au katika kipindi cha ujauzito husaidia kuupa mwili na mtoto virutubisho mbalimbali vilivyo na umuhimu katika kujenga na kulinda mwili.

Zingatia upate mafanikio bora.

Related Posts:

  • ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MTOTO MCHANGAHistoria ya ugumu wa kula, au mtoto hawezi kula kwa sasa. Historia ya mitukutiko, au mtoto anatukutika kwa sasa. Mtoto mchanga anaonekana mlegevu au amepoteza fahamu. Mtoto anasonga tu iwapo amesisimuliwa. Kupumua kwa haraka… Read More
  • MADHARA YA UPUNGUFU WA DAMU KWA MJAMZITOSehemu nyingine duniani, inakadiriwa kuwa karibu asilimia 4-16 ya vifo vinavyotokana na ujauzito husababishwa na upungufu wa damu. Aidha upungufu wa damu wakati wa ujauzito huongeza uwezekano wa madhara kwa mama na mtoto iki… Read More
  • FAHAMU KUHUSU FISTULA.fahamu kuhusu fistula Fistula ni nini?  Fistula ni shimo ambalo hutokea kati kati ya kibofu cha mkojo na uke au kati kati ya njia ya haja kubwa na uke wa mwanamke ambaye amejifungua kwa shida. Shimo hutokea pale amb… Read More
  • SABABU ZINAZOPELEKEA KUSHINDWA KUSHIKA UJAUZITO.HILI ni tatizo linalosababisha ugumba kwa wanawake kwa kiasi kikubwa. Wanawake wanaoshindwa kupata ujauzito hukabiliwa na matatizo matatu; * kwanza kabisa ni kuziba kwa mirija ya mayai kama tutakavyoona leo * matatizo katika… Read More
  • KUNAWA MIKONO NI AFYA.Wakina mama wengi wenye watoto wachanga hawana kawaida ya kunawa mikono Mara kwa Mara watakapo kumuhudumia mtoto. Yakupasa kunawa mikono kila Mara kwa kufuata utaratibu huu; *Kabla ya kunyonyesha *Kabla ya kumvisha au kumvua … Read More

0 comments:

Post a Comment

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR