Tuesday, July 18, 2017

Mimba kuharibika ni tukio linalopatikana mara nyingi katika wanawake na mamalia wa kike kutokana na shida mbalimbali katika ukuaji wa mimba tumboni mwa mama.

Ni tukio tofauti na utoaji mimba ambalo linasababishwa na binaadamu kwa makusudi.

Matukio yote mawili kwa kawaida yanaleta matatizo mbalimbali kwa mama.

Kuharibika kwa kijusi au kiinitete pengine kunatokana na mfadhaiko wa kiajali au sababu za kimaumbile. Mimba nyingi huharibika kutokana na kutonakiliwa kisahihi kwa kromosomu; pia huweza kuharibika kutokana na mazingira.

Mimba inayotamatika kabla ya wiki ya 37 katika kipindi cha ujauzito husababisha uzaaji wa mtoto na hujulikana kama kuzaliwa mapema

Kati ya 10% na 50% ya mimba hutamatishwa kwa njia zinazoweza kubainishwa kimatibabu, kutegemea umri na afya ya mwanamke mjamzito.

Mimba nyingi huharibika katika hatua za mapema sana za ujauzito, kiasi kwamba mwanamke hafahamu kwamba alikuwa mjamzito. Utafiti mmoja uliofanywa kupima homoni za kutoa yai na ujauzito uligundua kuwa 61.9% ya uhamili ulipotezwa kabla ya wiki 12, na 91.7% ya kuhabirika huko kulitokea bila ya dalili, na bila ya fahamu ya mwanamke aliyekuwa mjamzito. 

Hatari ya kutoka mimba ghafla hupungua kwa kiasi kikubwa baada ya wiki 10 kutoka kipindi cha mwisho cha hedhi. 

Kisababishi kikuu cha mimba kuharibika katika miezi mitatu ya kwanza huwa matatizo ya kromosomu ya kiinitete / kijusi, hali ambayo husababisha angalau 50% ya kutoka kwa mimba mapema. 

Sababu nyingine ni pamoja na magonjwa ya mishipa kisukari, matatizo mengine ya homoni, maambukizi, na matatizo ya chupa ya uzazi. 

Umri mkubwa na historia ya mimba zilizotangulia kuharibika ni sababu mbili kuu zinazohusishwa kwa pakubwa na mimba kuharibika ghafla. 

Hiyo inaweza pia kusababishwa na kiwewe kinachotokana na ajali.

Related Posts:

  • DALILI NA TIBA ZA UPUNGUFU WA DAMU KWA MJAMZITODalili Mjamzito mwenye upungufu wa damu wa kawaida mara nyingi anaweza asioneshe dalili zozote. Hata hivyo iwapo upungufu ni mkubwa, dalili za awali ni pamoja na uchovu wa mara kwa mara na kupumua kwa shida, kukosa hamu ya k… Read More
  • AINA ZA UZIBAJI WA MIRIJA YA UZAZIAINA ZA UZIBAJI WA MIRIJA Katika makala iliyopita Tuliona sababu kuu tatu zinazomfanya mwanamke asipate mimba. Kuziba kwa mirija ya uzazi huchukua asilimia ishirini ya tatizo la ugumba kwa mwanamke au mwanamke kupoteza uwezo … Read More
  • KUTOKWA UCHAFU UKENI NA TIBA YAKE.Kutokwa Na uchafu ukeni Ni sababu tosha itakayomfanya mwanamke asijisikie huru wakati wote! Kuna sababu nyingi zinazopelekea tatizo hili kutokea; Maambukizi katika uke ni tatizo la kawaida kwa wanawake na wanawake wengi wames… Read More
  • MAGONJWA YANAYOSABABISHA KUKOJOA USAHA, UUME KUWASHA AU KUUMA.KUNA magonjwa mengi yanayosababisha mtu kukojoa udenda (usaha), uume kuuma au kuwasha wakati wa kukojoa. Magonjwa yanayosababisha hali hiyo kwa sana ni pamoja na klamidia (chlamydia), kisonono (gonorrhea), trichomoniasis… Read More
  • MIMBA KUHARIBIKA NA SABABU ZAKEMimba kuharibika ni tukio linalopatikana mara nyingi katika wanawake na mamalia wa kike kutokana na shida mbalimbali katika ukuaji wa mimba tumboni mwa mama. Ni tukio tofauti na utoaji … Read More

0 comments:

Post a Comment

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR