Monday, July 17, 2017

Sehemu nyingine duniani, inakadiriwa kuwa karibu asilimia 4-16 ya vifo vinavyotokana na ujauzito husababishwa na upungufu wa damu.
Aidha upungufu wa damu wakati wa ujauzito huongeza uwezekano wa madhara kwa mama na mtoto ikiwemo kifo.

Madhara haya ni pamoja na Madhara kwa mama kipindi cha ujauzito:

kukonda au kuongezeka uzito kwa kiasi kidogo sana,

kuhisi uchungu kabla ya muda,

kondo la nyuma kutunga pasipostahili,

shinikizo la damu wakati wa ujauzito, na chupa kupasuka kabla ya wakati.

Madhara kwa mama wakati wa kujifungua:

kupatwa na uchungu usioeleweka na usio wa kawaida,

mtoto kuvuja damu ndani kwa ndani,

kupatwa na shock, hatari ya ganzi (anesthesia risk) kwa anayefanyiwa upasuaji,

moyo kushindwa kufanya kazi.

Madhara kwa mama baada ya kujifungua:

maambukizi baada ya kujifungua,

kizazi kushindwa kurudi katika hali ya kawaida au damu kuganda kwenye mishipa.

Madhara kwa mimba na mtoto atakayezaliwa:

Madhara ni pamoja na mtoto kuzaliwa njiti,

mtoto kuzaliwa na uzito mdogo,

mtoto kuwa na score ndogo (poor Apgar score), 

mtoto kuzaliwa akiwa amechoka (fetal distress),

Upungufu wa damu kwa mtoto, Watoto wanaozaliwa wakiwa na upungufu wa damu hukua kwa tabu, huwa na maendeleo duni ya kiakili na kimatendo (poorer intellectual developmental milestones),

uwezekano mkubwa wa kuwa na kasoro mwilini na hata kifo.

Kasoro hizo ni pamoja na matatizo ya magonjwa ya moyo yakuzaliwa nayo.

Kila mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika kipindi cha ujauzito ili kuepusha madhara haya.

Related Posts:

  • KUNAWA MIKONO NI AFYA.Wakina mama wengi wenye watoto wachanga hawana kawaida ya kunawa mikono Mara kwa Mara watakapo kumuhudumia mtoto. Yakupasa kunawa mikono kila Mara kwa kufuata utaratibu huu; *Kabla ya kunyonyesha *Kabla ya kumvisha au kumvua … Read More
  • MADHARA YA UPUNGUFU WA DAMU KWA MJAMZITOSehemu nyingine duniani, inakadiriwa kuwa karibu asilimia 4-16 ya vifo vinavyotokana na ujauzito husababishwa na upungufu wa damu. Aidha upungufu wa damu wakati wa ujauzito huongeza uwezekano wa madhara kwa mama na mtoto iki… Read More
  • MLO KAMILI KWA MJAMZITOLishe wakati wa ujauzito ni muhimu kwa ajili ya afya yako na maendeleo mazuri ya mtoto anayekua tumboni. FUATA MLOLONGO HUU KUWA NA LISHE BORA; 1.Jitahidi upate mlo kamili kila siku kwa kupata vyakula vya wanga, protini, mafu… Read More
  • ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MTOTO MCHANGAHistoria ya ugumu wa kula, au mtoto hawezi kula kwa sasa. Historia ya mitukutiko, au mtoto anatukutika kwa sasa. Mtoto mchanga anaonekana mlegevu au amepoteza fahamu. Mtoto anasonga tu iwapo amesisimuliwa. Kupumua kwa haraka… Read More
  • SABABU ZINAZOPELEKEA KUSHINDWA KUSHIKA UJAUZITO.HILI ni tatizo linalosababisha ugumba kwa wanawake kwa kiasi kikubwa. Wanawake wanaoshindwa kupata ujauzito hukabiliwa na matatizo matatu; * kwanza kabisa ni kuziba kwa mirija ya mayai kama tutakavyoona leo * matatizo katika… Read More

0 comments:

Post a Comment

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR