Sunday, August 27, 2017

Magonjwa ya zinaa ni magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiyana (sexually transmitted diseases),inayosababishwa na bakteria,virus au fungus wanaopenda ishi sehemu ya maji maji au unyevu unyevu katika mwili ,kama mdomoni,kooni,sehemu za siri au sehemu ya hajakubwa.

Iwapo mtu atakutana kimwili na mtu mwenye maambukizi hapo ni rahisi kuambukizwa. Magonjwa ya zinaa yanampata mwanamke na mwanaume pia kwa njia ya mdomo,uuke au uume.

Magonjwa ya zinaa yapo ya aina tofauti kuna

Kaswende

Kisonono

Gonorea

Ukimwi

Klamidia

Malenge lenge sehemu za siri

Dutu za sehemu ya siri

Magonjwa ya zinaa ni hatari kwa afya ,mama mjamzito akipata ugonjwa wa zinaa atapata dalili tofauti tofauti kama zifuatazo

Kuvimba sehemu za siri

Maumivu makali pindi ufanyapo mapenzi au wakati wa kukojoa

Kupata homa

Kutokwa vijipele ukeni vinaweza kuuma au visiume

Kupungua uzito

Maumivu ya mgongo

Kutokwa majasho kwa wingi nyakati za usiku

Kutokwa maji maji ukeni yenye harufu au isio na harufu

Kutokwa damu au usaha ukeni

Kuwashwa sana

Uke kubadili rangi

Madhara ya magonjwa ya zinaa kwa mama na mtoto

Mtoto anaweza kupata upofu

Uziwi-kushindwa mtoto kusikia

Mwanamke au mwanamme anaweza kuja kushindwa kuzaa sababu ugonjwa utaenda kuadhiri sehemu za uzazi

Kuziba mirija ya uzazi

Kifo

Ulemavu kwa mtoto

Mtu kupoteza kinga ya mwili kuwa dhoofu,kuumwa mara kwa mara.

Tiba

Magonjwa ya zinaa yanatibika iwapo  yatatibiwa mapema isipo kuwa ukimwi peke yake hauna tiba,mambukizi mengine mama mjamzito atatibiwa kwa kupewa antibiotic, mtoto  iwapo ataadhirika kipindi mama yake anamimba  baada ya kuzaliwa atawekwa dawa machoni ya kusafisha na kutibu.

 MTOTO ALIEPATA MAAMBUKIZI KUTOKWA KWA MAMA ,KAWEKEWA DAWA MACHONI

Iwapo mama amegundulika anamaambukizi na muda wa kijifungua umekaribia itabidi azalishwe kwa c-section ( operation)ili kumwepusha mtoto kupata maambukizi.

 

U.T.I / fungus ni magongwa ya infection nayo yanaweza mpata mama ila yenyewe hupati kwa njia ya kujamiiana haya yanatokana na virus na bakteria pia ambao unaweza watoa vyoo vya public au nyumbani iwapo mkiwa hamsafishi vyoo vizuri na kutumia maji safi ya kujitawazia.

 Uwapo mjamzito yakupasa kuwa makini Na kila hali.

1 comment:

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR