Sunday, August 20, 2017

Miongoni mwa vitu vikubwa ambavyo humtisha mwanadamu, yawezekana kifo kikawa ni namba moja, Ukifuatilia kwa ukaribu hali ambazo husababisha vifo ni pamoja na ajali, jinsia, majanga mbalimbali, umri, imani pamoja na magonjwa.

Hata hivyo vifo vitokanavyo na magonjwa ndio huchukua nafasi kubwa sana, Je umeshawahi kujiuliza upo salama kiasi gani ? Kutana na orodha ya magonjwa ambayo husababisha sana vifo !
    

1.Lower respiratory diseases(magonjwa ya chini ya upumuaji)
magonjwa Haya huathiri mfumo wa upumuaji wa chini kutokea kwenye trachea,bronchi na mapafu mfano wa magonjwa haya ni pneumonia, majipu kwenye mapafu(lung abscesses) na bronchitis (uvimbe kwenye bronchi).
Mwaka 2015 kulikuwa na wagonjwa milioni 291 na ulisababisha vifo million 2.74
Magonjwa Haya husababishwa na virusi au bakteria.

2.Magonjwa ya kuhara
Ni gonjwa la kwa kuua watu katika nchi znazoendelea hasa watoto chini ya miaka mitano, kila mwaka watoto chini ya miaka mitano 525000 hufariki kutokana na magonjwa haya.
Magonjwa haya yanatibika na kuzuilika, huweza kuyazuia kwa kunywa maji safi na usafi kwa ujumla.

3.Kiharusi
Kiharusi hutokana na sehemu ya ubongo kukosa damu na oksijeni kutokana na kuziba kwa mishipa ya ateri ya damu au kupasuka kwa mishipa ya damu.
4.Ischaemic heart disease
Huu ni ugonjwa wa moyo unaotokana na mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo kuziba kutokana na rehemu(cholesterol) kugandia kwenye mishipa ya damu ya moyo.

5.Ukimwi
Kwa mwaka 2016 inakadiriwa kulikua na vifo milioni 1 vilivyosababishwa na sababu zinazoambatana na VVU,pia inakadiriwa watu milioni 36.7 walikuwa wakiishi na VVU duniani.

6.Kifua kikuu
Mwaka 2015 watu milioni 10.4 waliugua TB na watu milioni 1.8 walikufa kutokana na TB,laki 4 kati ya hao walikua na VVU
Asilimia 95 ya vifo vya TB hutokea katika nchi zinazoendelea.

7.Malaria
Shirika la afya duniani (WHO) linakadiria mwaka 2016 watu milioni 212 walikua na malaria huku watu 429,000 wakifa kwa malaria,
Malaria husababishwa na plasmodium na kuenezwa na mbu.

8.Preterm birth
Watoto ambao huzaliwa kabla ya miezi 9 ya ujauzito,inakadiriwa watoto milioni 15 huzaliwa kabla ya miezi 9 kila mwaka.
Kuzaliwa kabla ya miezi 9 ya ujauzito ni kati ya sababu zinazoongoza kwa kusababisha vifo vya watoto chini ya miaka mitano.

9.Birth asphyxiation
Hii ni hali inayotokana na kukosa oxygen watoto kwa muda mrefu pindi wanazaliwa, hivyo husababisha matatizo ya kimwili hasa ubongo.
Asilimia 99 ya vifo hivi hutokea katika nchi zinazoendelea.

10.Ajali za barabarani.
Watu milioni 1.25 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na ajali za barabarani .
Ajali ndio huongozaa kwa kuua watu wenye umri wa miaka 15 hadi 29 huku asilimia 90 ya vifo hivi hutokea katika nchi zinazoendelea.

Bara la Africa ndio muhanga mkubwa wa vifo hivi na hii ni kutokana na uhaba wa wataalamu, vitendea kazi na utambuzi wa thamani ya mwili kwa binadamu mwenyewe, hata hivyo ikiwa u miongoni mwa wagonjwa wa magonjwa tajwa hapo juu, usikihofie kifo cha msingi zingatia ushauri wa wataalam au fika hospital mapema iwezekanavyo.

Zingatia ajali zinaua.

0 comments:

Post a Comment

Dondoo Zilizosomwa Sana hapa leo..!!

VIDEOS BAR